Ads

Wakenya wadai mwanzilishi wa Facebook anafanana na Yesu.....


Mark Zuckerberg sio mwana wa Mungu lakini baadhi ya watu wanamdhania kufanana sana na Yesu 

Mwanzilishi wa Facebook Mark Zuckerberg alifika Nigeria bila kutarajiwa Jumanne Agosti 30. Alishangaza wengi kwa kukimbia Lagos asubuhi na kuzuru watu mashuhuri baadaye.

Alifika pia Nairobi Alhamisi pia bila kutarajiwa.

Ana ufuasi mkubwa na ni mtu maarufu, baadhi ya sababu zinazowafanya baadhi ya watu kufikiria kijana huyo mwenye umri wa miaka 32 anafanana na Yesu.

Sababu zingine za kufikiria hivyo ni hizi

Uyahudi
Mark Zuckerberg anajivunia Uyahudi na hajaficha hisia zake kuhusiana na dini hiyo.

 Mtu wa kawaida
Ingawa ni mmoja kati ya watu walio tajiri zaidi ulimwenguni, utapatana naye akitembea mitaani kama mtu wa kawaida akiwa amevalia shati yenye mikoni mifupi na jinzi, kama Yesu tu. Ni mtu anayependa kutoa hasa kwa watu maskini, kama alivyofanya Yesu.
 Kuongea mbele ya umati
Yesu alikuwa na uwezo wa kuvutia umati kumsikiza na Zuckerberg ana sifa ya aina hiyo.
 Ufuasi
Mabilioni ya watu wanatumia Facebook, Instagram and WhatsApp, uvumbuzi wake kijana huyo. Yesu alikuwa na wafuasi wengi sana.
Huwa hafuati utaratibu

Zuckeberg huchukia itifaki kama alivyofanya Yesu ambaye hakupenda kufuata taratibu na protokali

Unadhani ni kweli?

No comments

Theme images by andynwt. Powered by Blogger.