Ads

Marekani mbioni kukabiliana na tisho la Korea Kaskazini

Marekani kuizuia Korea Kaskazini kuwa na silaha za nyuklia
Haki miliki ya picha
Mshauri wa maswala ya usalama wa rais Donald Trump amesema kuwa Marekani na washirika wake wako katika harakati kutatua tatizo na Korea Kaskazini kabla ya taifa hilo kuafikia mipango yake ya kinyuklia.
H-R McMaster alikuwa akizungumza katika mkutano wa ulinzi mjini Carlifonia ambapo alionya uwezekano wa vita dhidi ya Korea Kaskazini unaendelea kuongezeka kila uchao.
Hata hivyo aliongezea kuwa kuna njia za kutatua mzozo huo bila ya kutumia vita.
Ameitaka China kuiwekea vikwazo vya mafuta taifa hilo ili kufanya kuwa vigumu kwa Pyongyang kujaza mafuta makombora yanayofanyiwa majaribio.
Korea Kaskazini imeishutumu Marekani kwa kuchochea vita.
Imetaja zoezi la pamoja la kijeshi kati ya Korea kusini na Marekani kuwa la uchochezi na kwamba linaweza kusababisha vita.
Uwezo wa mkombora ya Korea Kaskazini
Uwezo wa mkombora ya Korea Kaskazini

No comments

Theme images by andynwt. Powered by Blogger.