Ads

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMATANO OCT 18

Christiano RonaldoHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionChristiano Ronaldo
Mshambuliaji wa Real Madrid Christiano Ronaldo, 32, anamtaka mshambuliaji wa Manchester United Marcus Rashford kujiunga na Madrid.(Don Balon in Spanish)
Mchezaji wa safu ya kati wa Manchester United Juan Mata, 29, amekataa mshahara wa pauni 375,000 kwa wiki kujiunga na ligi kuu ya China. (Daily Mail)
Meneja wa zamani wa Leicester Nigel Pearson haonekani kama mtu ambaye anaweza kuchukua usukani wa klabu hiyo kufuatia kufutwa kwa Craig Shakespeare (Leicester Mercury)
Meneja wa Wales Chris Coleman, 52, ambaye anamaliza mkataba wake mwezi ujao, anatakuwa huru kwa mazungumo kuhusu nasafi iliyo huko Leicester. (The Sun)
Jose MourinhoHaki miliki ya picha
Meneja wa Manchester United Jose Mourinho amekataa kutangaza msimamo kuwa atasalia na klabu hiyo siku za usoni (Guardian)
Meneja wa Chelsea Antonio Conte, amekiri kuwa alijaribu kumsaini mchezaji wa kiungo cha kati Radja Nainggolan, 29, kutoka Roma wakati wa majira ya joto.(Daily Express)
Aliyekuwa meneja wa England Sam Allardyce, anasema anataka kuenda kufanya kazi nchini Marekani. (ESPN)
Haki miliki ya picha
Newcastle United hawajapinga kuwepo mazungumzo na mfanyabiashara Amanda Staveley kuhusu kununuliwa kwa klabu hiyo. (Evening Chronicle)
Southampton wako kwenye mazungumzo na Barcelona kuhusu kuhama mshambuliaji Paco Alcacer, lakini wanakabiliwa na ushindani kutoka Lille ya Ufaransa.(Mirror)
Aston Villa wanaripotiwa kumwinda kipa Joe Lewis,30, kutoka Aberdeen. (Birmingham Mail)
Mchezaji wa kiungo cha kati wa Liverpool Roberto Firmino,26, alizuiwa kwa muda kuingia uwanja wa Mariborbaada ya kusahau kitambulisho chake. (Express)
Haki miliki ya picha
Meneja wa Liverpool Jurgen Klop amemuambia Alex Oxlade-Chamberlain, 24 kuwa hatacheza katika safu ya kati kati hivi karibuni. (Daily Mail)
Mejeja wa England Gareth Southgate anatathinia kumuita Jay Rodriguez,28, kutoka West Bron kujiunga na kikosi chake. (Telegraph)
Barcelona wana nia ya kumsaini mshambuliaji raia wa Brazil wa umri wa miaka 16 Lincoln kutoka Flamengo. (AS - in Spanish)

No comments

Theme images by andynwt. Powered by Blogger.