Ads

IGP Siro atoa mtaji wa biashara kwa jambazi sugu


Mkuu wa Polisi nchini Kamanda Simon Sirro amempa mtaji wa kufungulia  duka la mitumba jambazi aliyekuwa  tishio mjini Tanga kwa zaidi ya miaka 25 baada ya kuacha kazi hiyo.


Jambazi huyo  anayefahamika kwa jina la  Nuni Dunduu (Sirro mdogo) amewataka  vijana  wanaondelea kujihusisha  na kazi hiyo waache mara moja  .

Alisema   baada ya  kujisalimisha katika ofisi ya  Kamanda  huyo wa Polisi alimpatia  mtaji  na kwasasa ni mfanyabiashara wa  mitumba katika  soko  la  Mgandini .

‘’Mwaka 2009 wakati Sirro akiwa kamanda wa polisi mkoani hapa alinipatia kiasi cha Sh 50,000 kama mtaji wa biashara nikaanza kukaanga mihogo na baada ya kuona naumia kwa moshi nikaamua kuuza mitumba ambayo mpaka leo ndiyo kazi yangu’’alisema na kuongeza

“ Wakati nikiwa  jambazi nilikuwa naishi kwa wasiwasi  nikimuona hata mtu anakuja karibu yangu  nilikuwa naogopa najua  kanifuata  mimi, hivyo  kazi  hiyo inakufanya  uishi  kwa uoga na kama mkimbizi  kwani  unakuwa huna imani na mtu yeyote” Alisema  Nuni

Aidha  alisema  kuwa  anamshukuru   Sirro  kwani  yeye ni  mtu ambaye  amemfanya  kwa sasa aweze  kuishi maisha  mazuri  na  huru  kama  raia wengine  wa Tanzania  pamoja  na kumuwezesha  kufanya  biashara hiyo ambayo kwasasa inampatia kipato.

IGP sirro  alithibitisha  kumpokea ofisini kwake  kijana  huyo ambaye alikuwa jambazi sugu na  kusema kwasasa wamekuwa marafiki wazuri  na  amekuwa  mtiifu na mzalendo kwa  nchi yake.

Sirro aliwataka majambazi  wengine ambao bado wanaendelea na kazi  hiyo waache kazi hiyo na wajisalmishe  kama  alivyojisalimisha  Nuni  ambaye  alimpa  jina  la sirro mdogo , aliongeza  kuwa  mmemuona  Sirro Mkubwa  na Sirro Mdogo kwa sasa mtu huyu anaitwa Sirro mdogo.

Nuni alisema kilichomfanya aache ujambazi ni baada ya wenzake wengi kupoteza maisha huku wengine kufungwa jela   jambo ambalo lilimfanya aishi kama mkimbizi ndani ya nchi yake.

‘Hizo ni sababu ambazo zilinifanya   kwenda  kujisalimisha mwenyewe  kwa  Kamanda wa Polisi Mkoa  wa  Tanga  wakati huo  alikwa  ni  Kamanda  Simon Sirro ambaye ni IGP kwa sasa’’alisema

Akizungumzia Suala  la Kibiti  alisema  kuwa  Kibiti kwa  sasa kuko  shwari  na aliwataka waandishi  wa  habari  wawaeleze  wakazi  wa tanga wasiogope  kwenda  kibiti  kwani  kwasasa  kuko shwari .

“ Nendeni Kibiti  msiogope  kwasasa  kuko  shwari watu  wale wabaya  wameshaondoka  katika eneo la kibiti ’’ Alisema Sirro.

 “ Naziomba  zile kamati  za ulinzi  na  usalama  kuanzia  ngazi  zote  za  kijiji  mpaka mkoa  kufatilia  habari  za waharifu  na  kutoa taarifa kwa  vyombo  husika kwani watu hao sio  wazuri wamebadilika wamekuwa  wanyama  na wanamuua  mtu  yeyote ambaye hajagombana na bila sababu ya msingi” Alisema IGP Sirro.

Akizungumzia  suala la  kukamatwa  Wanasiasa  alisema wao kama  Jeshi la Polisi wanakamata  watuhumiwa   ambao wanaamini wamefanya makosa  ya jinai  lakini wakifanya upelelezi  wakigundua  mtuhumiwa hana kosa  wanamuachia na . Tukina tuhuma  ni za kweli tunampeleka mahakamani .

No comments

Theme images by andynwt. Powered by Blogger.