Ads

Aliyempiga mbunge wa Republican risasi auawa Marekani...

Police investigate a shooting scene after a gunman opened fire on Republican members of Congress during a baseball practice near Washington in Alexandria

Haki miliki ya picha
Mtu mwenye silaha ambaye aliwafyatulia risasi wabunge wa Republican wakati wakifanya mazoezi ya mchezo wa baseball mjini Washington DC ameuwa.
Kinara wa walio wengi bungeni Steve Scalise, ni mmoja wa wale waliojeruhiwa wakati wa kisa hicho cha mapema asubuhi katika hustani huko Alexandria , Virginia.
Mshambualiaji ambaye ni mzaliwa wa Illiois James T Hodgkinson, mwenye umri wa miaka 66, aliuawa baada ya ufyatulianaji wa risasi na polisi.
Waliojeruhiwa ni pamoja na polisi wawili.
Hodgkinson alikuwa amemfanyia kampeni mgombea urais wa Democratic Bernie Sanders.
House Majority Whip Steve Scalise (R-LA)Haki miliki ya picha
Ukurasa wa Facebook ambao unaonekana kuwa wa Bwana Hodgkinsion, umejaa propaganda dhidi ya Republican na Trump.
Bwana Sanders ambaye ni Seneta wa Vermont amesema amehusunishwa na kitendo hicho cha Hodgkinson.
Rais wa Marekani Donald Trump ametaja shambulia hilo kuwa la kinyama.
a victimHaki miliki ya picha
Trump alimtembelea bwana Scalise ambaye alipiwa risasi kwenye nyonga na yuko hali mahuti baada ya kufanyiwa upasuaji.
Hospitali ilisema kuwa Bwana Scalise alivunjika mifupa, na kupata majeraha ya viungo vya ndani na hivyo atahitaji upasuaji zaidi.
A mugshot of Alexandria shooting suspect James T Hodgkinson.Haki miliki ya picha

No comments

Theme images by andynwt. Powered by Blogger.