Ads

Marekani yaituhumu Syria kwa kuchoma wafungwa gerezani...........

Picha ya gereza hilo iliyopigwa kwa Satelite

Marekani imeituhumu serikali ya Syria kwa kujenga sehemu ya kuchoma maiti katika jela ya kijeshi iliyopo karibu na Damascus ili kuficha mauaji ya halaiki ya wanaoshikiliwa na serikali.
Wizara ya mambo ya nje ya Marekani imeonyesha picha zilizopigwa kupitia njia ya Satelite ambazo imesema ni sehemu ya kuchoma maiti katika gereza lililopo Sednaya ambapo Umoja wa Mataifa na mashirika ya kutetea haki za binadamu yamesema maelfu ya wafungwa wameteshwa na kunyongwa.

Sehemu inayosemekana kuwa wafungwa huchomewa

Mwanadiplomasia mwandamizi wa Marekani anayehusika na masuala ya Mashariki ya kati, Stuart Jones, amesema kwa siku wafungwa takriban hamsini wanauawa katika gereza la Sednaya.
Ameongeza kusema kuwa, mauaji hayo yanafanyika kutokana Syria kuungwa mkono na Urusi na Iran.

No comments

Theme images by andynwt. Powered by Blogger.