Ads

Marekani kugharamia mtambo ya kujikinga Korea Kusini

Marekani kugharamia mtambo ya kujikinga Korea Kusini


Haki miliki ya picha

Korea kusini inasema kuwa Marekani imekubali kulipa dola bilioni moja za kujenga kinga ya dhidi ya makombora ya Korea Kaskazini.
Awali rais Trump alikuwa amesema Korea kusini itagharamia ujenzi huo.
Maafikiano hayo yanajiri baada ya washauri wa maswala ya usalama wa mataifa hayo mawili kuzungumza kwa njia ya simu.
Ngao hiyo maalum ambayo inajengwa kwa sasa inalenga kudungua makombora yote yanayofyatuliwa kutoka Korea kaskazini.
Marekani imekubali kufadhili mradi huo kifedha huku korea kusini ikitakiwa kutoa ardhi.
Namna mfumo wa ulinzi wa THAAD unavyofanya kazi


No comments

Theme images by andynwt. Powered by Blogger.