Ads

Wanaotafuta baba za watoto wao,kutaja waliofanya nao mapenzi huko ujerumani....

Wizara ya sheria Ujerumani inapendekeza sheria mpya ambayo itawalazimisha wanawake wanaoshinikiza kutambua baba ya wanao kutoa taarifa ya wanaume waliofanya mapenzi nao wakati wa kutunga mimba. Hatua hii inawalinda wanaume ambao wamekua wakitoa ada ya malezi ya watoto ambao baadaye hugunduliwa ktokuwa wao. Huenda mwanamume kama huyo akalipwa fidia ya kulea mtoto asiye wake kwa miaka ishirini. Waziri wa sheria wa Ujerumani, Heiko Mass amesema wanawake watakubaliwa tu kutotambua wapenzi wao ikiwa itabainika kabisa kwamba wanaume wanaotakiwa kutoa ada ya malezi ni baba halisi ya wanawe. Hata hivyo sheria hiyo lazima ipitishwe na baraza la mawaziri na bunge kabla ya kuidhinishwa kuwa sheria.

No comments

Theme images by andynwt. Powered by Blogger.