Ads

Kumbe utovu wa nidhamu kwa wachezaji ndiyo chanzo cha kushuka kwa thamani ya soka la hapa Tanzania......


Image result for TFF


            Hivyo ndivyo mambo yalivyo
Sikuzote zote mkubwa hakanywi lakini huelekezwa ili ajirekebishe, na hivi ndivyo ilivyo kwa timu za wenzetu huko ulaya.Ambapo imeonekana kuwa nidhamu  ya wachezaji uwanjani ndiyo inazifanya timu na ligi za ulaya kuonekana bora ulimenguni.

Imeonekana kuwa kwa wachezaji wa timu za huko majuu(ulaya) wamekuwa wakionyesha nidhamu kwa kipindi  chote wakiwa na makocha wao uwanjani, mazoezini na hata kwenye vyumba vya kubadilishia nguo tofauti na baadhi ya wachezaji wa hapa Tanzania.Baadhi ya wachezaji wameonekana kutokuwa na nidhamu hasa wanapokuwa uwanjani nahii kupelekea sifa mbaya kwa ligi za mpira hapa nchini.

Akizungumza na 24 hours blog moja kati ya mdau  wa mpira hapa Tanzania Bw Mussa Ramadhani maarufu kwa jina la Ramso The Blues ambaye ni shabiki wa timu ya Chelsea ya huko uingereza alisema kuwa, amekuwa shabiki wa timu hiyo(Chelsea)kwa muda mrefu sana na hivyo kugundua kuwa timu zinazoshiriki ligi ya uingereza(EPL) ikiwemo Chelsea wachezaji wake wana nidhamu ya hali ya juu na hicho ndicho kinacho ifanya ligi hiyo kukubalika ulimwenguni.

Mussa  alifunguka nakuelezea kuwa, kwa Tanzania iko tofauti kabisa kwani mchezaji anaweza kuvunja sheria za soka(mpira) na kuamua kufanya chochote anachojiskia.Kwa mfano mchezaji anaweza kumpiga refa uwanjani hii yote nikukosa nidhamu na pia mchezaji anapoeleweshwa kwa kosa alilolifanya hujiona yeye yupo sahihi na kusimamia upande wake.Lakini kitendo hiki ndo chanzo cha kuharibu mpira wa hapa Tanzania na pia kushuka kiwango kwa wachezaji.

Mussa aliongezea kuwa, licha ya nidhamu wachezaji wa timu za huko majuu huwa wanacheza mpira kwa jitihada zote kwa kuwa wanajua ndiyo ajira(kazi) yao tofauti na wachezaji wa hapa Tanzania wanacheza mpira ili kuonekana na sio kuwa wanacheza kama kazi na hiki  kinachowafanya wenzetu kuwa juu.

“kiujumla wachezaji wa timu za huko majuu wana nidhamu lakini licha ya nidhamu huwa wanacheza mpira kwa jitihada zote kwa kuwa wanajua ndiyo kazi yao.Tofati na wachezaji wa hapa Tanzania wanacheza mpira ili kuonekana na sio kuwa wanacheza mpira kama sehemu ya kazi na hiki  kinawafanya wenzetu kuwa juu siku zote” Moja kati ya mashabiki wa timu ya Chelsea hapa Tanzania Bw mussa Ramadhani alisema;

Yapo matukio ambayo yanatendeka ndani ya uwanja yasiyo yakinidhamu nahii ni kwenye michezo mbalimbali ya ligi kuu Tanzania bara(VPL) halikadhalika michuano mingine lakini kutokana na uongozi(TFF) kutofuatilia kwakina matukio haya ndo mana mara nyingi huwa yanajirudia.

January 2016 mchezaji Juma Nyoso(Mbeya City) alifanya kitendo kisicho cha nidhamu  kumzalilisha mchezaji mwenzake wa timu ya Azam John Bokko na uongozi  ulichukuchukua uamuzi wa kumfungia kutocheza mpira(mechi) hata moja mwaka mzima wa 2016.



24 hours blog                                                                        imeandaliwa na ally mshana

No comments

Theme images by andynwt. Powered by Blogger.