Haya ndio yamemfanya 20% kupotea kwenye game......
Kama unakumbuka jana
tuliishia baada ya 20% kupata tunzo hapo ndipo pakawa mwanzo way eye kupotea
kwenye game.Haya hebu leo tuangalie nikwanini na nini chanzo cha jamaa kupotea
kwenye game hii ya muziki wa bongo flava.
Ilikuwa ni mwezi tarehere 8
Machi PER alipoweza kupiga story na gazeti la Mwanasport na ndipo
nilipogundua kwanini jamaa alipotea.Wakati
stori zikiendelea 20% aliweza kufunguka mengi ambapo mashabiki zake
wakisika hawawezi kuamini lakini huwa siku zote ukweli unadumu milele hivyo hakuamua
kuficha kitu na ndipo alipoamua kumwaga mambo hadharani.
PER alisema kuwa huwa yeye sio mtu wakutoa nyimbo za bandika
bandua hapana bali yeye anatoa nyimbo baada ya muda Fulani kupita na huo
niutaratibu ambao amejiwekea na ndoma huwa anaonekana tofauti na wasanii wengine pia nakusema kuwa
kutoa nyimbo hovyohovyo nikuwachanganya
mashabiki.
“Kitendo
chakutoa nyimbo bila mpangilio kinaweza kunifanya nisitoe nyimbo bora hivyo sima muda maalumu wa kutoa
nyimbo kuwa inachukuwa muda gani, pia huwa kuna nyimbo
nyepesi na ngumu hivyo inategemea na muda wakuchimba mashairi halisi”,
“Uandishi
nikitu ambacho kama ilivyo kwangu unajua
kuandika huwezi kubadilisha na hivyo ndivyo ilivyo kwangu kwani
nafahamu naandika nini na kwawakati gani mana kama
niuwezo wa kuandika mashairi ninao tena mzuri”20% alifunguka.
20% wakati stori zikiendelea ndo akagusa kidonda ambacho
maumivu yalishaanza kupotea na kusema kuwa jambo lililosababisha yeye
kushuka baada yakuchukua tunzo
tano kwenye tunzo zinazotolewa kila mwaka hapa nchini Kilimanjaro Music
Awards na kuwaacha midomo wazi watu wengi ni niuvutaji wa bangi
“Wakati
ule nilikuwa ni mtu wakuitikia kila kitu, umri pia nao ulichangia hivyo baada
ya tunzo ndipo mambo
yalipojitokeza ya aina tofauti tofauti,
kupigwa vita kulizidi na ndivo watu walipoanza kunifaahamu undani wangu na kunizibia kilanjia”
“Nilikuwa
najaribu kuangalia haya maisha yakuitikia yanaweza kuisha kwa muda gani watu ambao walikuwa wananifahamu walinifahamu
kiundani baada ya tunzo hizo,hivyo nilianza kuangalia
ni nini.Nilipochoka kuitikia niliamua kuuliza
maisha hayo yataisha lini,nilianza
kuuliza jinsi yakusaka pesa na inatoka
wapi hio niliwauliza mameneja wangu ambao
kumbe hakufurahishwa na maswali yangu.
Baada
ya kuuliza hilo ndipo utata ulipozidi, hasa hawa wanaojiita mameneja ,mameneja wa bongo wanataka msanii awe
chini yake kwakila kitu, wakati msanii ndie anayemuajiri meneja.Hilo wengi
hawalikukubali wanataka kupelekeshwa na walio wengi hawakupi mwongozo
mzuri wa maisha zaidi yakukufanya
uendekeze starehe ambazo zinakuharibu
na ndio inakuwa furaha kwao" yote hayo kaeleza PER
Japo 20 kafunguka juu ya kilichomfanya kushuka kiwango chake
cha mziki lakini asikuambie mtu kumbe alizushiwa mambo mengi yaliyonfanya
kuumia mpaka leo hii.leo sikuambii kesho tutajua 20 alizushiwa kitu gani
kinachomfanya kuumia hadi leo hii
Usikose kutembelea
24
hours blog kwa habari na story zadi
24 hours blog na Ally msahana
No comments