Ads

Hii hapa historia ya Mpira wa miguu kwa kwaz ufupi.......

Image result for mpira



Siku zote huwa napenda kusema mzoa asili haiachi asili na kama huamini basi hutokaa ukaja kuamini hata siku moja. Kila kitu unachokiona ndani yua hii dunia basi ujue lazima kiwe na asili yake.

hebu leo tuiangalie hii historia ya mpira wamiguu japo kwa uchache ili uamini kuwa wahenga hawakukosea kusema "mzoea asili haachi asili"

Michezo mbalimbali ya kuchezea mpira inaweza kupatikana katika kila uwanja wa jiografia na historia. Wachina, Wajapani, Wakorea na Waitalia wote walikuwa wakicheza mpira zamani kabla ya enzi zetu. Wagriki na Waromania walitumia michezo hiyo kuwaandaa wapiganaji kabla ya vita. Hata hivyo, ni nchini Uingereza ambapo umbo la sokala kisasa lilianza kuibuka.

Ilianza wakati mashirikisho mawili (Shirikisho la Mpira wa miguu na Mpira wa Ragbi) yalitawanyika. Shirikisho la kwanza lilibakia Uingereza. Mnamo Oktoba 1963,Vilabu 11 vya London vilituma wawakilishi katika mkutano wa Freemason ili kujadili na kuweka kanuni zilizokubalika kusimamia mechi zilizochezwa kati yao.

Mkutano huu ulipelekea kuanzisha kwa Shirikisho la Kandanda (Football Association).
Miongoni mwa kanuni zilizowekwa ni zile za kukataa utumiaji wa mikono kushika mpira na kunyanganya kwa nguvu. Soka na Ragbi zilitawanyika mnamo tarehe hii.

Miaka minane baada ya kuanzishwa, Shirikisho la Kandanda (FA) lilikuwa na wanachama 50. Shindano la kwanza la kandanda lilianza mwaka huo- Kombe la FA- ambalo lilifuatiwa na lile la Ligi ya Ubingwa miaka 17 baadaye. Wachezaji wawili wa Kilabu ya Darwin, John Dove na Fergus Suter walikuwa wa kwanza kulipwa kwa mchezo wao. Kitendo hiki kilikuwa mwanzo wa soka ya kulipwa iliyohalalishwa mnamo mwaka wa 1885. Mwamko huu ulipelekea kuanzishwa kwa Mashirikisho ya kitaifa nje ya Uingereza (Great Britain). Baada ya Shirikisho la Kandanda la Uingereza, Mashirikisho yaliyofuatia ni yaUskoti (1873), Wales (1875) na Eire (1880).

Kutokana na ushawishi mkuu wa Uingereza katika mataifa ya Dunia, Soka ilizambaa kote duniani.Mataifa mengi mengine yalianzisha Mashirikisho ya Kandanda kufikia 1904 wakati Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) lilipoanzishwa. Tangia hapo, kandanda ya kimataifa imekuwa ikikua licha ya vikwazo mbalimbali. Kufikia 1912, FIFA ilikuwa na uanachama wa mashirikisho 21, idadi iliyoongezeka na kufika 36 kufikia 1925. Kufikia 1930- mwaka ambapo kwa mara ya kwanza kulikuwa na mashindano ya Kombe La Dunia, FIFA ilikuwa na wanachama 41. Idadi hii ilizidi kuongezeka na kufika 51 mnamo 1938 na 76 kufikia 1950. Baada ya Kongamano la FIFA la mwaka 2000, kulikuwa na wanachama 204 na idadi hii inazidi kukua kila mwaka.


24 hours blog



1 comment:

Theme images by andynwt. Powered by Blogger.