Ads

Yaaweza kuwa Zari ndo chanzo cha kifo cha Ivan...




Nasema haya kutokana na sababu nitakazo zihainisha hapa chini ila ukweli kifo cha Ivan Semwanga chanzo chake nimapenzi sababu kuu ni Zari!

Ukiangalia tangu waachane na Zari Ivan hakuikubali ile hali na alijitahidi kumbembeleza Zari ila Zari hakutaka!

Na Ivan alitegemea Zari angerudi waendelee na maisha! ila baada ya kuzaa na Diamond Ivan alizidi kuishiwa tumaini la kuwa na Zari kwani alimpenda mno!!

Katika hizi picha alikuwa akituma ujumbe kwa Zari! Rudi mama kama pesa ipo huku!pia ukumbuke Diamond alipost kuwa amenunua Hammer kesho naye aapost ana Hammer3 hii yote nikuwa alimpenda sana Zari!

Pia katika kuachana Ivan hakuwahi kupost picha yoyote akiwa na mwanamke! aliamini hakuna mwanamke wakumchallenge Zari hivyo hakuona sababu yakujidhalilisha kwani alijua Zari ni mzuri sana, hivyo hakaona ajipe muda!na alitamani arudi ila maamuzi haya, hayakuwa upande wake!! kwani Zari alishamchoka!. Hivyo umauti huo umetokana na msongo mkubwa wa mawazo!. Nina hakika Mungu akimfungulia Zari kutafakari juu ya kifo cha Ivan atatambua yeye ndiye aliyesababisha!

Mara nyingi tukiwa katika mahusiano ya muda mrefu hutokea tunachokana na kutamani yavunjike hata kama tunawatoto!kutokana na maudhi madogo madogo!ila ujidanganya nakusema bora tuachane ila wakiondoka! baada ya wiki utamani kuwarudisha ila mara nyingi uogopa watu watanionaje!!mbaya wakienda ambapo hatuwezi kuwaona tena kama kufariki basi hapo ndipo huwa tunapatwa msongo wa mawazo!! na hasa kama wametuachia watoto!. 

Taadhari ikikutokea usijixhanganye katika pombe tumia muda kukaa na familia na kuwa busy na watoto baada ya muda tafuta mwenza japo atakuwa halingani na yule na nivigumu kumpata kama yule!na mhalalishe mbele ya familia yako ili upate muda wakukaa naye ndani kuliko kutumia muda mkiwa hotelini!maana ukirudi kitandani kwako hali itaanza upya!

Hivyo nirudi katika mada kifo cha Ivan Semwanga kimesababishwa na msongo wa mawazo ya mapenzi juu ya Zari.

No comments

Theme images by andynwt. Powered by Blogger.