Ads

Waasi waonyesha wasiwasi kusitishwa mapigano nchini Syria........

Marekani na Urusi zinaongoza kuhamasisha kusitishwa kwa vita

Makundi ya waasi nchini Syria yameonesha kutoridhishwa na kusitishwa kwa mapigano kunakosimamiwa na Urusi na Marekani ambapo kusitishwa huko kunatarijiwa kuanza Jumatatu jioni.
Makundi hayo yanatakiwa kusema kama watajiunga kwenye makubaliano hayo ama la.
Kuna madai kuwa moja ya kundi la waasi la Ahrar al-Sham watakataa kusitisha mapigano hayo.
Miundombinu na majengo vimeharibiwa vibaya
Kiongozi wa kikundi kingine cha waasi mjini Alepo amesema kuwa wanakubali kuondoa uhasama na kuruhusu misaada lakini ana wasiwasi na makubaliano.
Mashambuzli ya ndege za Syria na Urusi yameendelea siku ya jumapili katika mji wa Alepo na Idlib.
Zaidi ya watu 100 wameuawa katika mashambulizi yaliotekelezwa siku ya jumamosi.

No comments

Theme images by andynwt. Powered by Blogger.