Ads

Kabla ya Manchester derby, wafahamu wachezaji 7 waliowahi kucheza Man United na Man City

Image result for EPL CUP
Ni marachache kushuhudia wachezaji kuhamia kwenye klabu hasimu hususan kama timu ni za mji mmoja. Lakini tangu Bob Milarvie alipovichezea vilabu vyote vya Manchester United na Manchester City, wachezaji 24 wameshacheza kwenye vilabu vyote vya jiji la Manchester.
Idadi hiyo ya wachezaji wameiwakilisha Manchester United na Manchester City kwa miaka kadhaa, lakini mchezaji maarufu zaidi ni anabaki kuwa Denis Law.
Billy Meredith, Peter Barnes na Brian Kidd, ni miongoni mwa wachezaji waliozichezea timu zote za Manchester.
7. Peter Beardsley – Mshambuliaji

peter-beardsley2

Manchester United: 1982-1983
Mechi: 0 Magoli: 0
Manchester City: 1998 (kwa mkopo kutoka Bolton)
Mechi: 6  Magoli: 0
Peter Beardsley aliitumikia Manchester United msimu wa 1982-83 lakini hakufanikiwa kucheza mechi yoyote ya ligi (wakati huo First Division)
Tangu alipoondoka Old Trafford, nyota huyo wa England alicheza kwenye vilabu vingine sita ikiwa ni pamoja na Liverpool kabla ya kujiunga na Manchester City kwa mkopo akitokea Bolton Wanderers.
6. Carlos Tevez – Mshambuliaji
carlos-tevez2
Manchester United: 2007-2009

Mechi: 63  Magoli: 19
Manchester City: 2009-2013
Mechi: 105  Magoli: 57
Carlos Tevez kwa mara ya kwanza alijiunga na Manchester United kwa mkopo akitokea West Ham na akafanikiwa kuonesha uwezo mkubwa, na kujizolea idadi kubwa ya mashabiki kutokana na uwezo wake mkubwa wa kupambana.
Uhamisho wake kutoka United kwenda kwa majirani zao Man City kulifanya awe mchezaji wa kwanza kutoka Old Trafford moja kwa moja tangu Terry Cooke alipofanya hivyo mwaka 1999.
5. Owen Hargreaves – Kiungo
owen-hargreaves2
Manchester United: 2007-2011

Mechi: 27  Magoli:2
Manchester City: 2011-2012
Mechi: 1  Magoli: 0
Owbwen Hargreaves ulikuwa ni usajili mkubwa kutoka Bayern Munich na aliisaidia United kutwaa taji la mabingwa Ulaya lakini majeraha yaliharibu maendeleo yake ndani ya Old Trafford.
Baada ya mkataba wake kumalizika alifanya maamuzi magumu ya kujiunga na wakali wa Etihad Stadium lakini alifanikiwa kucheza mchezo mmoja tu wa Premier League kabla ya kustaafu kutokana na sababu za majeruhi.
4. Andy Cole – Mshambuliaji
andy-cole1
Manchester United: 1995-2001

Mechi: 195  Magoli: 93
Manchester City: 2005-06
Mechi: 22  Magoli: 9
Andy Cole alikuwa ni mfungaji wa aina yake kwenye kikosi cha United baada tu ya kusajiliwa akitokea Newcastle United mapema mwaka 1995.
Ni miongoni mwa wachezaji wa kikosi kilichotwaa mataji matatu ndani ya msimu mmoja (Treble), alifunga bao dhidi ya Tottenham na kuisaidia United kutwaa taji huku mshambuliaji huyo mzaliwa wa Nottingham akatimkia Blackburn Rovers na Fulham kabla ya kujiunga na Manchester City mwaka 2005.
3. Terry Cooke – Kiungo
terry-cooke2
Manchester United: 1994-1999

Mechi: 4  Magoli: 0
Manchester City: 1999-2002
Mechi: 37  Magoli: 7
Cooke ni zao la timu ya vijana ya Manchester United, mwaka 1995 alifunga mkwaju wa penati ulioipa ubingwa wa FA timu ya vijana. Alicheza mechi nne za Ligi kuu England akiwa kwenye kikosi cha wakubwa.
Cooke was a part of the Old Trafford youth Class of ’92 alongside David Beckham, Paul Scholes, Gary and Phil Neville, Nicky Butt and Ryan Giggs.
Cooke alikuwa ni miongoni mwa vijana waliolelewa Old Trafford miaka ya 1990 na wachezaji kama David Beckham, Paul Scholes, Gary and Phil Neville, Nicky Butt pamoja na Ryan Giggs.
2. Andrei Kanchelskis – Winger
andrei-kanchelskis3
Manchester United: 1991-1995

Mechi: 123  Magoli: 28
Manchester City: 2001 (kwa mkopo kutoka Rangers)
Mechi: 10  Magoli: 0
Andrei Kanchelskis alisajiliwa na United akitokea Shakhtar Donetsk na kuisaidia United kutwaa taji la EPL mwaka 2093 na jingine msimu uliofuata.
Mwaka 1995 aliuzwa kwenda Everton lakini muda mfupi baadaye alihamia Fiorentina. Klabu hiyo ya Serie A ilimtoa kwa mkopo kwenda City mwaka 2001 na akacheza mechi 10.
1. Peter Schmeichel – Golikipa
peter-schmeichel2
Manchester United: 1991-1999

Mechi: 292  Manchester: 0
Manchester City: 2002/03
Mechi: 29  Magoli: 0
Peter Schmeichel alikuwa nahodha wa United wakati kikosi hicho kikitwaa mataji matatu mwaka 1999 huku akitajwa kuwa golikipa bora katika historia ya klabu hiyo.
Raia huyo wa Denmark alijiunga na Sportinglakini baadaye akarudi kutoka Lisbon na kutua Aston Villa miaka kadhaa baadae.
Chakushangaza, alijiunga na Manchester City na kuendeleza rekodi ya kutofungwa kwenye mchezo wa Manchester derby.
Shafii Dauda

No comments

Theme images by andynwt. Powered by Blogger.