Ads

Harmoniza huenda ni baba kijacho....

Nimeyapokea mengi Leo June 4 ila moja kati ya hayo ni pamoja na hili la staa wa Bongofleva kutoka WCB, Harmonize kuweka wazi juu ya ujio wa mtoto wake.
Harmonize ambaye stori zilizokuwa mitaani ni kwamba baada ya kuachana na mrembo Jackline Wolper sasa hivi yupo na mzungu, aliandika kwenye ukurasa wake wa Instagram 
”Mnh! nawaza huu mchanganyiko wa damu ya kimakonde na ya kizungu sijui itatuletea mwana gani… asa nikiona kakomwe hapo, kananistua😁…Chonde mtoto chukua vyote kwangu ila kwenye rangi jitahidi uibe ya mama yako…..!!! nikavimbe Mtwara 😊

Siku ya June 3 Harmonize alipost picha ya msichana mwenye asili ya kizungu na kuandika >>>👪 💕💕 UJINGA WAKATI WA KWENDA Post iliyoashiria kuwa huyo ni mpenzii wake wa sasa.
source millard ayo....

No comments

Theme images by andynwt. Powered by Blogger.