Mtu aliyewaua watu 5 Marekani akamatwa
Polisi katika jimbo la Washington nchini Marekani wamemkamata mshukiwa mmoja kuhusiana na kisa ambapo watu watano walipigwa risasi na kuuwawa katika jengo moja la kibiashara siku ya Ijumaa.
Wamemtaja mshukiwa huyo kwa jina Arcan Cetin mwenye umri wa miaka 20.
FBI wameongeza kusema kuwa bado hakuna ushahidi kuwa lilikuwa tukio la kigaidi.
Kiini cha mauaji hayo yaliyotokea katika jumba la biashara kwenye mji wa Burlington bado hakijulikani. Aidha polisi wanasema kuwa mshukiwa huyo hana historia ya kuwa na uhusiano na makundi yenye siasa kali
No comments