Ads

Majambazi 14 Wameua Askari Wanne Dar es Salaam...


Watu wanaoaminika kuwa ni majambazi usiku huu wamevamia Benki ya CRDB iliyopo Mbande wilayani Temeke mjini hapa na kuua askari kisha kupora silaha na kutokomea kusikojulikana.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro alipoulizwa kuhusu tukio hilo, amesema hawezi kuzungumza chochote kwa maelezo kuwa yuko eneo la tukio na amesema atafutwe kesho.

Uhalifu huo umetokea ikiwa umepita mwaka mmoja tangu kutokea kwa tukio la majambazi kuua askari wanne na kupora silaha baada ya kuvamia kituo cha Polisi Stakishari, Ukonga jijini hapa.

No comments

Theme images by andynwt. Powered by Blogger.